Beki US Monastir amuhofia Fiston Mayele

Beki wa US Monastir ya Tunisia Ousmane Adama Ouattara amesema, wapo tayari kwa mchezo wa Mzunguuko wa kwanza Hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya Mabingwa wa Tanzania Young Africans.

Miamba hiyo itakutana Februari 12 mjini Tunis-Tunisia, katika mchezo wa Kundi B, huku kila upande ukihitaji kuanza vizuri hatua hiyo, kwa kuokota alama tatu muhimu.

Ouattara, ambaye aliwahi kucheza AS Vita 2019-2021, amesema wanatambua Young Africans ni timu nzuri na ina Mshambuliaji hatari Fiston Mayele, hivyo wanapaswa kuwa makini wakati wote wa mchezo huo.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii