Kocha Graham Potter Akiri Chelsea Ndiyo Kazi Ngumu Zaidi Katika Soka

Kocha Graham Potter anadai kuwa ana kibarua kigumu zaidi katika taaluma yake ya soka huku mazimwi ya majeraha ikivamia klabu ya Chelsea. 


Kikosi cha Potter kwa sasa kinajikokota katika nafasi ya 10 kwenye msimamo wa Ligi Kuu Uingereza, mkufunzi akikabiliwa na presha ya kutimiza matarajio ya mmiliki wa Blues Todd Boehly. 


Akichukuwa mikoba ya kunoa klabu hiyo kutoka kwa Thomas Tuchel aliyetimuliwa mnamo Septemba 2022, kocha huyo wa zamani wa Brighton sasa anakabiliwa na hatari ya kupigwa kalamu miezi minne tu baada ya kuajiriwa. 

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii