Mbunge "Yanga hii inatoboa CAF"

Kocha wa timu ya Bunge (Bunge SC), Ahmed Juma Ngwali amekiangalia kikosi cha sasa cha Yanga kisha akatamka kibabe kwamba kama wataamua kukaza watatoboa kiulaini tu katika michuano ya CAF na hata Ligi Kuu Bara msimu huu.


Ngwali ambaye ni mbunge wa Wawi, anayemiliki Leseni B ya ukocha wa soka, huku akiwa amewahi kuichezea timu ya Taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes, alisema amekifuatilia kikosi cha Yanga kwa msimu huu na kuona kina mabadiliko makubwa tofauti na msimu uliopita.


Alisema kwa hali hiyo anaamini kama kitakaza msuli hasa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, basi kina nafasi ya kufanya vizuri zaidi kulinganisha na msimu uliopita kilipokwama raundi ya kwanza kwa kutolewa na Rivers United ya Nigeria iliyoifumua nje ndani kwa bao 1-0 kila mchezo.


Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii