Saratani Yaua Watu 25,000 kwa Mwaka

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa saratani umeua watu 25,000 mwaka 2020 na kuufanya ugonjwa huo kuwa tishio zaidi ya Uviko-19 iliyoua watu chini ya 1,000 hapa nchini.

Waziri Ummy amesema Serikali imeiomba jumuiya ya kimataifa kushiriki katika mapambano ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwa ni miongoni mwa hatua ambazo zimechukuliwa kukabili ugonjwa huo.

Waziri Ummy amesema hayo leo Jumatatu Septemba 26, 2022 jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa taarifa ya Taasisi ya The Lancert Oncology ya hali ya ugonjwa wa saratani katika nchi zilizo usini mwa Jangwa la Sahara kwa upande wa Afrika Mashariki.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii