BABA Mtakatifu na mkuu wa kanisa katoliki duniani Papa Francis (85) amewateua maaskofu 20 na kuwatawaza kuwa makaldinali watakaoongezeka kwenye jopo litakaloshiriki kumteua mrithi wa kiti chake.
Papa Francis katika uteuzi wake huo alijaribu kuwapa kipaumbele makaldinali wa jamii zilizotengwa zaidi. Mmojaa wa waliochaguliwa ni Askofu Hyderabad Anthony Poola kutoka nchini India mwingine ni Askofu Peter Ebere Okapaleke kutoka Nigeria.
Hafla hiyo ya kuwatawaza Maaskofu hao ilifanyika katika kanisa la St.Peters huko Vatican. Katika waliotawazwa 16 kati yao wana umri chini ya miaka 80.