SIMBA WAGOMEA KIKAO NA WAANDISHI WA HABARI.

UONGOZI wa klabu ya Simba kupitia kwa kitengo cha habari kinachoongozwa na Ally Shantri ‘Chico’ wamegoma kufanya kikao cha kocha na waandishi wa habari kisa bango lenye nembo ya GSM.

Mkutano wa makocha kwa ajili ya mchezo wa kesho wa Simba na Yanga ulikuwa unafanyika leo katika makao makuu ya Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF).

Kocha wa Yanga, Nassredine Nabi ndiye aliyeanza kuzungumza na alipomaliza msemaji wa TFF, Clifford Ndimbo aliwataka Simba waingie lakini waligoma.

Chico alisikika akisema ”toeni bango kwanza”.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii