YANGA imemalizana na
Bernard Morrison akisaini mkataba wa mwaka mmoja kurejea klabuni kwa
masharti kadhaa lakini kuna balaa kubwa wanalifanyia kazi kwa usiri
mkubwa.
Yanga imeweka wazi kwamba wanashusha mastaa watano wa kigeni na jina kubwa jingine ni Mrundi Gael Bigirimana.
Ni
kiungo ambaye ukihesabu timu alizocheza Ulaya inashtua kidogo lakini
Mwanaspoti limejiridhisha kwamba kupitia Cedrick Kaze na wakala wake
Yanga inapambana kumshawishi atue Tanzania.
Amepitia klabu kama
Coventry City, Newcastle United, Rangers na sasa Glentoran ya Ireland ya
Kaskazini. Matajiri wa Yanga, GSM wako katika mazungumzo ya kumrudisha
Afrika, Bigirimana ambaye ni tegemeo kwenye timu ya Taifa ya Burundi
amewahi kutamba na Newcastle United ya England ambayo anaishabikia Rais
mstaafu Jakaya Kikwete.