Aliyekuwa Kiungo wa Klabu ya Sofapaka Wisdon Naya Aaga Dunia

Aliyekuwa kiungo wa klabu ya Sofapaka Wisdom Naya ameaga dunia, klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Kenya (KPL) imethibitisha kupitia kwa taarifa.
Aliyekuwa Kiungo wa Klabu ya Sofapaka Wisdon Naya Aaga Dunia
Mamake Dinah Cherop vilevile alithibitisha kifo cha mwanawe na kusema kuwa kilitokea jioni ya Alhamisi, Julai 14.
Naya ameaga dunia kufuatia matatizo yaliyotokana na kukatwa mguu wake baada ya kupoatikana na ugonjwa wa saratani.
Hali ya mguu huo kukatwa inaaripotiwa kuathiri sehemu zingine za mwili wake.
"Tunasikitishwa kumpoteza kiungo wetu wa zamani Wisdom Naya. Kinda huyo ameaga dunia kutokana na saratani eneo la goti lake. Rambirambi zetu kwa familia na marafiki wa Naya. Ampumzike pema," Sofapaka imesema kupitia kwa taarifa.
Naya alishinda tuzo ya mchezajo bora zaidi katika mashindano ya Copa Cocacola ya Bara Afrika mwaka 2016 kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 16 akichezea Shule ya Upili ya St Anthony.
Alijiunga na klabu ya Sofapaka mwaka 2019 lakini akalazimika kukaa nje ya uwanja katika kile ambacho madaktari walidhani ni jeraha la goti. Alitengana na Sofapaka mwaka 2020 baada ya msimu mmoja pekee.
Vipimo vilidhihirisha kuwa alikuwa na uvimbe wa saratani kwenye goti lake na akaanza kupokea matibabu katika hospitali ya Eldoret Oncology.
Baadaye Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Moi mjini Eldoret ilimpaa rufaa hadi hospitali moja nchini India kukatwaa mguu uliokuwa ukiugua.
Baada ya kufanyiwa upasuaji uliofana nchini India, alirudi Kenya mnamo Januari 14 kuanza safari yake ya kupona.
Lakini hakufanikiwa kurejea katika hali sawa kwani jioni ya Alhamisi aliaga dunia kutokana na matatizo yaliyotokana na kukatwa mguu huo.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii