WAKALA APELEKA JINA LA NABI SIMBA

INAWEZA kuwa habari ya kushtua sana kwa mashabiki wa Yanga, lakini ndivyo ilivyo kwamba wakala wa Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi, alilipelekea jina la kocha huyo kwa mabosi wa Simba ili kumtafutia kazi mpya.

Za Ndaani Kabisa, zinasema kuwa wakala huyo alilipelekea jina la Nabi kwa vigogo wa Msimbazi, baada ya awali klabu hiyo kuchomoa kumchukua ilipokuwa ikisaka kocha wa kuziba nafasi ya Sven Vandenbroeck aliyekuwa ametangaza kuachia ngazi siku chache baada ya kuifikisha timu hiyo makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu uliopita.

Taarifa hizo zinasema Simba ilimkataa Nabi na kumchukua Didier Gomes aliyekuwa amepishana na Nabi ndani ya El Merreikh ya Sudan.

Gomes alijiondoa El Merreikh ilipotinga makundi na nafasi yake kuchukuliwa na Nabi ambaye alikaa kwa muda mchache kabla ya kufurushwa baada ya kuboronga makundi ikiwamo kutoka suluhu na Simba mjini Khartoom katika mechi zao za makundi msimu huo.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii