Wafananisha bomu la ardhini na Magimbi Kenya

Bomu la ardhini la enzi za ukoloni ambalo halijalipuka lilmegunduliwa katika kijiji kimoja katikati mwa Kenya ambapo baadhi ya wakazi walidhania kuwa ni mzizi wa mboga za kienyeji.

Polisi wa Kenya walisema wanakijiji wanaohusika walikusanyika karibu na kitu hicho, wengine wakihoji "kuwa ni kombora huku wengine wakidai kuwa ilikuwa mizizi ya mboga iliyokua sana".

Maafisa wa Kurugenzi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), walienda mara moja mara baada ya kupewa taarifa na kubaini kitu hicho kuwa ni bomu. "Kuna uwezekano mkubwa liliachwa na vikosi vya Uingereza wakati wa ghasia za Mau Mau Mwaka 1953, ambapo sehemu za misitu ya Mlima Kenya na Aberdare zilikumbwa na mashambulio ya angani, ili kuwaondoa wapiganaji wa Mau Mau," ofisi ya DCI ilisema

Bomu hilo lilipaswa kulipuliwa kwa usalama siku ya Jumatatu, DCI ilisema.

Wakenya wamekuwa wakilinganisha kisa hicho na kile kilichotokea wiki kadhaa dhidi ya simba aliyedhaniwa kupotea katikati mwa Kenya.

Maafisa wa wanyama pori wa Kenya waliitwa kwenye eneo hilo baada ya mfanyakazi wa shamba kuona kile alichofikiri ni simba aliyejificha chini ya kichaka kwenye ukingo wa boma hilo.

Lakini ikawa ni mfuko tu na picha kubwa ya kichwa cha simba juu yake.

Hata hivyo, Katika tukio la hivi punde zaidi, kile kilichofikiriwa kuwa mboga ya mizizi maarufu kiligeuka kuwa "sheria hatari ya kijeshi", kulingana na polisi.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii