IMF yaunda mfuko wa ufadhili kukabiliana na changamoto za muda mrefu

Shirika la fedha ulimwenguni IMF limeidhinisha kuundwa kwa mfuko mpya wa ufadhaili unaolenga kuzisaidia nchi za kipato cha chini na za kati kukabiliana na changamoto za muda mrefu ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi na milipuko ya majanga. Mkuregenzi mtendaji wa IMF Kristalina Georgieva ametangaza uidhinishwaji wa mfuko wa ustahimilivu utakaonza kutumika mwanzoni mwa mwezi Mei, ukilenga kukusanya dola za Kimarekani bilioni 45. Mfuko huo mpya utaruhusu mataifa matajiri zaidi kuelekeza akiba zao za dharura ili kusaidia nchi zilizo hatarini kushughulikia changamoto za muda mrefu. Kwa hivi sasa, IMF inatoa kiwango cha chini cha riba kusaidia nchi kukabiliana na changamoto za muda mfupi, kama vile mfumuko wa bei na changamoto za muda za kifedha. Ufadhili huo utayalenga mataifa yaliyoathiriwa zaidi na janga la corona.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii