NYUMBA 4000 JIMBO LA MPENDAE WAPOKEA MKONO WA FUTARI KUMUENZI MAREHEMU SALIM TURKEY

WAKAZI wa Jimbo la Mpendae Visiwani Zanzibar wamepata faraja Kwa familia ya Marehem Salim turkey Kwa kuendeleza yale mazuri kwa wananchi wake hususani kuwakumbuka watu wenye uhitaji katika kipindi cha Mfungo wa Ramadhani.

Akizungumza na Michuzi Tv Mtoto wa Marehem Salim turkey, ambae ni Mbunge wa jimbo hilo Toufiq Salim amesema mara Kwa mara wakati wa Mwezi wa Ramadhani Marehemu alikua akiwakumbuka watu wenye uhitaji na kugawana nao kidogo anachopata.

"Wananchi walijua hatutaweza kuendelea na utaratibu huo lakini kutokana na misingi mizuri aliyoacha mpendwa wetu, jukumu hilo tumelibeba sisi familia yake na Leo tumegawa Mkono wa futari Kwa takribani watu 4000 katika Jimbo la Mpendae hapa Visiwani Zanzibar."

Aidha Miongoni mwa vitu vilivyogaiwa Kwa watu hao ni pamoja na vyakula mbalimbali ikiwemo Mchele, Maharage,mafuta, Sukari,unga pamoja na pesa.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii