Taylor Swift Ang’ara Kwenye ‘Date Night’, Avaa Gauni La Tsh Milioni 7.2

Msanii maarufu wa muziki nchini Marekani, Taylor Swift, ameonekana akiwa na mume wake, Travis Kelce, katika ‘date night’ jijini New York, huku akivutia kwa muonekano wake mpya pamoja na gauni lenye thamani ya takribani TSh milioni 7.2.

Wanandoa hao, wote wenye umri wa miaka 36, walitoka Jumapili, Septemba 6, 2026, na kwenda kupata chakula katika mgahawa maarufu wa Kihindi, Ambassadors Clubhouse New York, uliopo eneo la NoMad, Manhattan.

Swift alivaa gauni refu la hariri lenye mistari kutoka kwa mbunifu Stella McCartney, likiwa na thamani ya takribani dola 2,800 (TSh milioni 7.2). Alikamilisha muonekano huo kwa mkoba wa mbunifu huyo pamoja na viatu vya Aquazzura vya rangi ya metali.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii