Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amemtembelea na kumjulia hali Rais Mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, katika makazi yake yaliyopo Mbweni, Unguja, Zanzibar.
Ziara hiyo imefanyika ikiwa sehemu ya kumjulia hali Rais huyo mstaafu na kuendelea kudumisha uhusiano na heshima kati ya viongozi wa kitaifa.