Ebola DRC: Maambukizi yapindukia 2,000 na vifo 796

Mlipuko wa ugonjwa wa Ebola huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo unazidi makali ambapo maambukizi yameongezeka na kufikia watu 2,073 na vifo 796.

Hayo ni kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na mamlaka za Kongo. Hayo yanaripotiwa wakati wahudumu wa afya huko Bunia, ambako ndio kitovu cha mlipuko huo wa Ebola  wakiripotiwa kugoma wakidai mishahara yao huku mashirika ya misaada yakionya kuwa hali hiyo inaweza kudhoofisha zaidi juhudi za kupambana na ugonjwa huo.

Hata hivyo, changamoto kubwa ni ufuatiliaji wa waliokutana na wagonjwa, huku Shirika la Afya Duniani WHO likitahadharisha kuwa mlipuko huo ni mkubwa zaidi kuliko inavyoelezwa.

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii