Katika kuelekea maadhimisho ya siku ya kuzuia
kuzama maji duniani jamii jijini mwanza imetakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia
usalama wao hasa wanapokuwa katika shughuli za uvuvi ili kuzuia vifo
vitokanavyo na kuzama maji.
Rai hiyo imetolewa hii leo na Marry Francis, afisa
uchechemuzi kutoka shirika la usimamizi
wa mazingira na maendeleo ya uchumi emedo
alipokuwa akizungumza na jembe habari ambapo amesema takwimu za kidunia
zinaonyesha kuwa takribani watu zaidi ya laki tatu wanapoteza maisha kutokana na
vifo vya kuzama maji, wazazi wanatakiwa
kuwaweka mbali watoto, na kuwa na
uangalizi wakati wa shughuli zozote za maji na hasa uvuvi.
Bi marry amesema kuwa takwimu hizo zilizotolewa na
shirika la afya ulimwenguni zinaonyesha kuwa
asilimia 92 ni uchumi wa kati na uchumi mdogo huku asilimia 59 ikiwa
vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa huku wavuvi wakiwa kwenye hatari kubwa
zaidi ya vifo vya kuzama maji
Aidha marry ametoa rai kwa jamii kuhakikisha inawalinda watoto dhidi ya
shughuli mbalimbali zinazohusiana na maji ili kuzuia vifo huku akiwasisitiza
watu kuvaa koti okozi muda wote wanapokuwa ndani ya maji pamoja na kufuata
taarifa za mamlka ya hali ya hewa pamoja
na kuimarisha vifaa na vyombo vyao vya uvuvi.
Maadhimisho ya siku ya kuzuia kuzama maji hufanyika kila mwaka duniani kote July 25 ambapo kauli mbiu ya mwaka huu 2026.