Maafisa wa Pakistan
wamefahamisha kwamba nchi hiyo imependekeza duru ya pili ya mazungumzo kati ya
Marekani na Iran kumaliza vita inayoendelea.
Pendekezo la Islamabad limetolewa wakati Marekani ikiweka
vizuizi kamili leo katika bandari za Iran, huku Makamu wa Rais wa Marekani JD
Vance akisema mazungumzo na Iran yamepiga hatua na Rais Donald Trump akionesha
jana Jumatatu kwamba Iran iko tayari kufikia makubaliano.
Pakistan yapendekeza awamu nyingine ya majadiliano ya
usuluhishi kati ya Iran na Marekani
Kwa upande mwingine, jana afisa mmoja mwandamizi wa kundi la Hezbollah alisema kundi hilo halitozingatia makubaliano ya aina yoyote ambayo yatatokana na mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Lebanon na Israel yatakayoanza leo huko Washington.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime