Papa Leo wa XIV ahimiza amani duniani

Kiongozi huyo wa juu zaidi wa kanisa katoliki duniani anaendelea na ziara yake barani Afrika akiwa katika siku ya pili katika kituo chake cha kwanza cha ziara hiyo nchini Algeria.

Kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki duniani Papa Leo wa XIV ametowa mwito wa amani na kumalizwa kwa tabia ya ukoloni mamboleo inayoendelea duniani.

Matamshi hayo ya papa aliyatowa mwanzoni mwa ziara yake nchini Algeria jana na kuandamwa na kauli za kushambuliwa vikali kwa maneno na Rais Donald Trump na makamu wake JD Vance, baada ya kukosoa vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.

Papa Leo XIV kufanya ziara mjini Annaba nchini Algeria

Aidha hivi leo kiongozi huyo wa kiroho anatarajiwa katika mji wa Annaba ambako atatembea kufuata nyayo za Mtakatifu Augustino, mwanatheolojia aliyekuwa na taathira kubwa katika Ukristo ambapo ataendesha misa katika kanisa kubwa la Mtakatifu Augustino mbele ya viongozi wa kanisa hilo kutoka barani Afrika.

Itakumbukwa kuwa Papa Leo ni kiongozi wa kwanza wa juu wa Kanisa Katoliki duniani kuitembelea Algeria, ambacho ni kituo cha kwanza cha ziara yake ya mataifa manne ya Afrika.

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii