Marekani imeondoa vikwazo dhidi ya kaimu rais wa Venezuela, Delcy Rodríguez, hatua inayotafsiriwa kama mabadiliko makubwa ya sera ya Washington kuelekea Caracas.
Hatua hiyo, iliyotangazwa na Wizara
ya Fedha ya Marekani, inaashiria kutambuliwa rasmi kwa uongozi wa Rodríguez baada ya kuondolewa
madarakani kwa kiomngozi wa nchi hiyo, Nicolás Maduro.
Hakuna sababu rasmi iliyotolewa kuhusu uamuzi huo, lakini
unaonekana kuwa sehemu ya juhudi za kurejesha uhusiano wa kidiplomasia kati ya
mataifa hayo mawili.
Rodríguez,ambaye aliwekewa vikwazo mwaka
2018, amepongeza hatua hiyo akisema ni mwanzo wa kuimarika kwa mahusiano na
kufungua milango ya uwekezaji na maendeleo ya kiuchumi nchini humo.
Marekani pia inatarajia kushirikiana na serikali mpya ya Venezuela kuongeza uzalishaji wa mafuta na rasilimali nyingine, huku nchi hiyo ikiwa na akiba kubwa zaidi ya mafuta duniani.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime