Zitambue Faida za Tufaha (Apple) katika Kulinda Moyo Wako

Unatambua kwamba ulaji wa tufaha (Apple) moja kila siku kunaweza kusaidia kuboresha afya ya moyo kwa kutanua mishipa ya damu, kupunguza uvimbe, kulinda seli, na kusaidia kuweka mishipa ya damu yenye afya, kulingana na utafiti wa karibuni.

Virutubisho Muhimu Vilivyomo Kwenye Tufaha

Tufaha ni tajiri kwa nyuzi za lishe (fiber) na misombo ya mimea inayosaidia kudumisha shinikizo la damu la kawaida na kazi bora ya moyo na mishipa. Zina:

  • Flavonoids: ikiwemo quercetin na proanthocyanidins

  • Asidi za phenolic

  • Nyuzi za lishe

Daktari wa moyo Dr. John Higgins (UTHealth Houston) anasema husaidia moyo kwa njia kadhaa:

1. Kupanua Mishipa ya Damu

Flavonoids huchochea mishipa ya damu kupanuka kidogo, na kufanya damu ipitie kwa urahisi zaidi.

2. Kupunguza Uvimbe

Antioxidants zinazojulikana kama polyphenols hufanya kazi kama viambato vya asili vinavyopunguza uvimbe, kupunguza msongo kwenye mishipa kwa muda, anasema Cassandra Lepore, mtaalamu wa lishe mjini New York.

3. Kulinda Seli

Antioxidants zilizopo kwenye tufaha husaidia kulinda mishipa ya damu dhidi ya uharibifu wa kila siku unaosababishwa na molekuli zisizo imara mwilini.

4. Kusaidia Mishipa ya Damu Iwe na Afya

Nyuzi zinazoyeyuka (soluble fiber) zinaweza kupunguza kiwango cha cholesterol na kudumisha unyumbufu wa mishipa, hivyo kusaidia kudhibiti shinikizo la damu kwa muda mrefu.

5. Kudhibiti Shinikizo la Damu

Hata hivyo Tufaha lina takribani mg 150 ya potasiamu kwa kila tunda linalosaidia unywaji wa potasiamu wa kila siku ambapo  Potasiamu husaidia kupumzisha kuta za mishipa ya damu, kupunguza shinikizo la damu, na kulinda misuli dhidi ya kuteseka au kucramp, kulingana na Harvard Medical School.

#10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii