Almasi nyeusi yenye umri wa mabilioni ya miaka yauzwa kwa dola milioni 3.16

Almasi nyeusi yenye umri wa mabilioni ya miaka inayoaminika kuwa almasi kubwa zaidi iliyokatwa duniani, imeuzwa kwa £3.16m.

Kwa jina la The Enigma, jiwe hilo la thamani ya karati 555.55 ambalo lina uzito sawa na ndizi, lilitarajiwa kuingiza zaidi ya £4.4m.

Dalali Sotheby's alisema "mnunuzi amechagua kutumia cryptocurrency kwa ununuzi."

Kuna nadharia zinazoshindana kuhusu asili ya jiwe, ikiwa ni pamoja na kwamba lilibebwa duniani na asteroid.

Baada ya mnada huo, mjasiriamali wa sarafu fiche Richard Heart alienda kwenye mitandao ya kijamii kudai kuwa yeye ndiye mnunuzi wa The Enigma.

Aliwaambia wafuasi wake zaidi ya 180,000 wa Twitter kwamba "mara tu malipo yanapopitishwa na milki kuchukuliwa" jiwe hilo la thamani litaitwa jina la "almasi HEX.com", akimaanisha jukwaa la blockchain aliloanzisha.

Jiwe hilo ni mojawapo ya aina ngumu zaidi za almasi ya asili.

Carbonados ni nadra sana na zimewahi kugunduliwa nchini Brazil na Jamhuri ya Afrika ya Kati pekee.

Kwa sababu vina osbornite, madini yanayopatikana tu kwenye vimondo, vinaaminika kuwa vinatoka angani.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii