YAS YAZINDUA KAMPENI YA “ANZIA ULIPO” KANDA YA ZIWA SAFARI YA KUWAWEZESHA WATEJA KUFIKIA NDOTO ZAO

Katika tukio maalum lililofanyika ndani ya Kanda ya Ziwa, kampuni ya mawasiliano ya YAS imezindua rasmi kampeni yake kubwa iitwayo “Anzia Ulipo”, kampeni inayolenga kuwawezesha Watanzania, hasa vijana na wafanyabiashara, kutumia teknolojia kufikia ndoto zao  popote walipo.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkurugenzi wa YAS  Kanda ya Ziwa, Bwana Joseph Mutalemwa, alisisitiza kuwa kampeni hii si ya kawaida, bali ni mwendelezo wa safari ya mabadiliko ambayo YAS imeanza tangu ilipozinduliwa rasmi Novemba mwaka jana, ikibadilika kutoka chapa ya Tigo hadi YAS.

“Hayakuwa mabadiliko tu ya jina. Tulibadilisha kabisa namna tunavyowasiliana na wateja wetu. YAS iko kwa ajili ya kumsaidia mteja kufanikisha maisha yake ya kila siku  awe ni kijana anayeanza biashara, mkulima kijijini, au mwanafunzi anayetafuta fursa kupitia mtandao,” alisema Mutalemwa.

 Katika hotuba yake, Mutalemwa alitaja mafanikio kadhaa ambayo YAS imepiga ndani ya miezi kadhaa tu, hasa katika upanuzi wa huduma za 4G na 5G ndani ya Kanda ya Ziwa. Kwa sasa, YAS inapatikana hadi maeneo ya vijijini kabisa – na kwa vifaa vinavyounga mkono teknolojia hizo, wateja wanaweza kufurahia huduma za kasi na uhakika.

 

“Sasa hivi hata ukienda kule kijijini kwa bibi yako, kama simu yako ina 4G, utapata 4G ya YAS. Na katika majiji  kama Mwanza, Kahama, Shinyanga na Geita, tumeweka 5G katika maeneo haya,” aliongeza.

 

 

 

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii