Mwanafunzi aliyechoma moto shule akamatwa

Baadhi ya majengo ya Shule ya Sekondari ya Jenista Mhagama iliyopo Halmashauri ya Songea yameungua kwa Moto ikiwemo Mabweni ya Wanafunzi wa kike na Stoo ambapo  imelidai  kuwa moto huo umetokana na hujuma

Mkuu wa Wilaya Wilman Ndile, alipoulizwa kuhusu tukio hilo amesema Moto umesababisha hasara kubwa na umeharibu majengo, Chakula cha Wanafunzi cha thamani ya Tsh. Milioni 1, vingine vilivyoungua ni Magodoro na Vifaa ya Umeme

Aidha DC amesema kuwa Mwanafunzi huyo alichoma Moto shule mara tatu kwa siku tofauti, Mei 31, Juni 1 na Juni 3, 2025, kwa sasa anashikiliwa na anatarajiwa kupelekwa Mahakamani na wemezungumza na Wazazi wake nao pia wamekiri kuwa Mtoto huyoa ni mkorofi.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii