Kikundi cha Utetezi wa Wanawake (Woman Change) Afrika Kusini kimeanzisha Kampeni ya kutaka kusitishwa kwa Tamasha lijalo la Msanii #ChrisBrown Nchini humo Disemba 14.2024 kwa madai ya kuwa anahistoria mbaya ya unyanyasaji wa kijinsia huku wakitaja hukumu yake kutokana na kumshambulia aliekuwa mpenzi wake 2009 #Rihanna
.
Tamasha hilo linaenda sambamba na Siku 16 za Kupinga Unyanyasaji wa Kijinsia nchini Afrika Kusini
.
Ombi la kupiga marufuku show ya #Brown limekusanya zaidi ya sahihi 20,000, huku mawakili wakiitaka Idara ya Masuala ya Ndani ya Nchi kumfutilia mbali viza yake.
.
Wakati mashabiki wengi, wakiwemo wanawake, wakiisubiri kwa hamu show ya #CB, wanaharakati wanasisitiza kuwa kumruhusu kutumbuiza kunadhoofisha mapambano dhidi ya ukatili dhidi ya wanawake.