Msanii wa muziki nchini ambae anafahamika kwa jina la Gachi amezua furaha na gumzo mitandaoni baada ya kupewa zawadi ya gari jipya jipya aina ya Range Rover, tukio lililowashangaza mashabiki wake wengi.
Taarifa zinasema kuwa Gachi alikabidhiwa gari hilo katika hafla fupi iliyohudhuriwa na watu wa karibu pamoja na baadhi ya wadau wa burudani, kama ishara ya kutambua mchango wake katika tasnia ya muziki na kazi zake zinazovutia mashabiki.
Baada ya kupokea zawadi hiyo, Gachi alionekana akiwa na furaha kubwa na kutoa shukrani kwa wote waliomfikiria, akisema kuwa hatua hiyo ni motisha kubwa kwake kuendelea kufanya kazi kwa bidii zaidi na kuboresha muziki wake.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime