Uchaguzi nchini Togo: Kambi ya rais yaridhika, upinzani watangaza kukata rufaa

Wakati mwelekeo na matokeo ya uchaguzi wa Aprili 29 nchini Togo yakitangazwa, upinzani na hasa Chama cha Dynamics for the Majority of the People (DMP) kinaendelea kushtumu ubadhirifu uliojitokeza katika uchaguzi huo.

Brigitte Kafui Adjamagbo-Johnson anakusudia kutumia haki zote ili aweze kutendewa haki, amesema hayo mbele ya mwandishi wetu wa habari huko Lomé, Peter Sassou Dogbé.

"Tuligundua kuwa kuna kura zilizotumiwa vibaya. Tunaweza kukuambia kuwa kulikuwa na baadhi kura ambazo zilikuwa tayari kuwekwa kwenye sanduku za kura nchini kote. Kando na mazoea ya kupiga kura kwa njia ya kawaida, kulikuwa na ujazo mwingi wa kura kila mahali. Hii ni aina fulani ya wizi mkubwa ambao tumeshuhudia. Kwa haya yote, tuna ushahidi. Tutachukua hatua na kuwashtaki wale waliohusika katika kitendo hiki. "

Chama tawala, Union for the Republic (UNIR), kilichotangazwa kuongoza kwa mwelekeo wa kwanza, kimefurahishwa na matokeo yake. Kwa mujibu wa mshauri mpya kabisa wa kisiasa wa Rais wa Jamhuri, anayehusika na mkakati wa kisiasa, Pascal Bodjona, alama hizi nzuri zinatokana na uwepo wa mara kwa mara wa chama kwenye uwanja. Na ikiwa kumekuwa na udanganyifu, mamlaka yenye uwezo itafanya kazi yao, amemwambia mwandishi wetu.

“Wale ambao wana uthibitisho kwamba kumekuwa na udanganyifu lazima, muda ukifika, wawasiliane na mamlaka husika (ili wafahamu) kuhusu mgogoro wa uchaguzi. Hata huko Lomé, UNIR ilipata kura nyingi, katika kihistoria yake. (Au) Lomé, ambayo ilionekana kwa muda mrefu kuwa ngome ya upinzani pia, imeshuhudia madai haya ya wizi.

Nadhani matokeo ambayo yanaonekana kwa chama cha UNIR yametokana na matunda ya kazi, unyakuzi wa ardhi, na kwa hakika wananchi wamefurahishwa na vitendo vilivyofanywa kwa muda mrefu."

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii