Dawa za kulevya, ulevi kupindukia chanzo matukio ya uhalifu

Matumizi ya dawa za kulevya na ulevi wa kupindukia wa baadhi ya watu katika jamii, vimetajwa kuwa ni sababu mojawapo inayopelekea wao kujiingiza kwenye utendaji wa matukio ya kiuhalifu.

Hayo yamebainishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi wa Polisi George Katabazi wakati akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake.

Amesema, “jamii tushirikiane kukemea matumizi ya dawa za kulevya kwani vijana wengi wakishatumia hujiingiza katika kufanya uhalifu hususani ukatili wa Kijinsia.”

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii