Miaka 30 jela kwa kumnajisi mtoto wa kambo

Mahakama ya Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga, imemuhukumu Makungu Juma (41) kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kumnajisi mtoto wake wa kambo mwenye umri wa miaka 12.

Hukumu hiyo, imetolewa na Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Christina Chovenye ambapo alisema adhabu hiyo imetolewa kwa kosa la kubaka kifungu 130 (1) (2)(e) na 131(1) kanuni ya adhabu sura namba 16.

Chovenye alisema kesi hiyo yenye namba 291 ya mwaka 2023 ilifunguliwa baada ya kuletwa shauri hilo mahakamani baada ya kutenda kosa mwezi Julai hadi Septemba mwaka 2023 kwa nyakati tofauti.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii