Idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na mafuriko yaliyotokea wilayani Hanang mkoa wa Manyara imeongezeka na kufikia watu 49 baada ya kupatikana kwa miili mingine miwili.
Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa mkoa wa Manyara, Queen Sendiga aliyoitoa leo Novemba 4, 2023 amesema idadi ya majeruhi bado ni 85.