WATU MATAJIRI BARANI AFRIKA

Licha ya mlipuko wa virusi vya corona, watu matajiri barani Afrika wameongeza utajiri wao zaidi ya walivyokuwa miaka minane iliopita.

Mabilionea wa bara hili kwa jumla walijipatia $84.9 bilioni ikiwa ni asilimia 15 zaidi ya utajiri wao miezi 12 iliopita na kwamba ni dadi kubwa iliyojumlishwa tangu 2014 ambapo kulikuwa na mabilionea 28 kulingana na jarida la Forbes.

Jarida la Forbes lilitumia bei za hisa na thamani ya ubadilishanaji wa fedha kuanzia Januari 19 2022 ili kupima utajiri wao.

Afrika Kusini na Misri ndio mataifa yenye mabilionea wengi, nchi zote mbili zikiwa na mabilionea watano kila mmoja zikifuatiwa na Nigeria yenye mabilionea watatu huku Tanzania ikiwa na bilionea mmoja ambaye ni mfanyabiashara Mohammed Dewji.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii