Mahakama katika Visiwa vya Shelisheli, imemsomea mashtaka ya uchawi kiongozi mkuu wa upinzani nchini humo, Patrick Herminie pamoja na watu wengine saba, akiwemo Mtanzania.
Herminie ambaye anatajwa kutaka kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa 2025 kwa tiketi ya chama kikuu cha upinzani, United Seychelles Party (USP) amekanusha madai hayo na kueleza kuwa ni mbinu ovu za kisiasa za kumchafulia jina lake na kumfanya ashindwe kugombea urais.
Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii