Neymar kujimwambafai Saudi Arabia

Kiungo Mshambuliaji kutoka nchini Brazil Neymar da Silva Santos Júnior ameamua kuachana na maisha jijini Paris, Ufaransa na kutimkia zake Saudia Arabia ambako anakwenda kulipwa kibosi zaidi.

Nyota huyo ameafikiana na Al-Hilal na jana jioni ilitarajiwa dili lake la Euro 160 milioni kwa miaka miwili linakwenda kumpa mkwanja wa maana zaidi katika masiha yake.

Kwa mujibu wa L’Equipe, PSG na timu hiyo ya Saudi Pro League wamefikiana makubaliano ya uhamisho wa Neymar, huku mwandishi mahiri Julien Laurens akiripoti kuwa Les Parisiens watapokea ada ya Euro 90 Milioni, huku muhusika akikubali mkataba wa miaka miwili.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii