Andre Onana akubali kukosolewa Man Utd

Mlinda Lango kutoka nchini Cameroon Andre Onana amekubali kukosolewa na mashabiki baada ya kuruhusu bao lake la kwanza Old Trafford kwenye mchezo wa mwisho wa kujiandaa na msimu dhidi ya Lens.

Hata hivyo, Manchester United ikaibuka na ushindi wa mabao 3-1 lakini kipa huyo alipondwa baada ya kushindwa kuzuia mpira wa mbali uliopigwa na mchezaji wa Lens, Florian Sotoca na kuingia moja kwa moja kwenye nyavu.

Baada ya mchezo huo kumalizika Onana alisema ataubeba mzigo wa lawama kichwani kwani ndio sehemu ya kujifunza kwa hiyo hatajali maneno ya mashabiki mitandaoni.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii