Katika tukio la Jumanne, Juni 27, watatu hao waliripotiwa kuzirai na kukosa hewa ndani ya tanki la maji taka lenye futi tisa, ambalo lilikuwa bado linaendelea kujengwa.
Akithibitisha kisa hicho, kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Nakuru Town Magharibi Francis Wahome alisema kuwa watatu hao, mwashi na msaidizi wake na mfanyakazi mwingine, walitumia kamba kuteremka ndani ya tanki hilo.