Urusi yafanya mashambulizi mapya ya anga mjini Kiev

Urusi imefanya wimbi jipya la mashambulizi katika mji mkuu wa Kiev mapema leo Jumanne huku milio ya ving'ora ikisika katika maeneo kadhaa ya Ukraine kama tahadhari.

Meya wa mji mkuu huo Vitali Klitschko ameandika katika mtandao wa Telegram juu ya mashambulizi hayo ya anga huku akiwataka wakaazi wa mji huo kutotoka nje.

Klitschko ameongeza kuwa mwanamke mwenye umri wa miaka 27 amekimbizwa hospitali baada ya kupata majeraha kusini magharibi mwa wilaya ya Holosiivskyi.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii