Katibu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Pwani – PUSA, Kelvin Nyambura amewataka Wanafunzi na Wazazi kuwa watulivu akisema vifo hivyo vimewagusa watu wengi na Taifa la Kenya kiujumla na kwamba bado wanafuatilia kuhusu madai ya Dereva kulalamika kuwa basi hilo lilikuwa na tatizo la breki.
Uongozi wa Chuo Kikuu cha Pwani umesema ajali hiyo imelikumba basi moja kati ya manne yaliyokuwa kwenye msafara wa wanafunzi 120, madereva wanne na afisa mmoja wa michezo kuelekea kwenye michezo, mjini Eldoret.
Mmoja wa Wanafunzi walionusurika katika ajali hiyo, Ian Okoth (22), alisema “tunataka chuo kikuu kituhakikishie usalama wa magari yetu kabla ya kwenda safari maana tumegundua kuwa dereva alikuwa akilalamika kuhusu breki ya gari.”