Uchungzi wa kifo cha June Jerop mwanafunzi wa chuo kikuu cha Kenyatta kinapoendelea siri fiche kuhusiana na mauaji ya mwanadada huyo zimeanza kuchipuka.
Jesse Wafula mshukiwa mkuu katika mauaji hayo katika nakala alizoziandikia mahakama kuu amesema kuwa Jerop alikuwa mfanyabiashara mwenza na kuwa alikuwa anatumia kampuni yake kufanya nayo kandarasi.
Wafula ambaye anatambulika kama mtaalamu wa maswala ya komputa ameiambia mahakama kuwa mwendazake alikuwa na deni lake la milioni moja lililotokana naye kuumuzia gari.
Mshukiwa katika ufichuzi wake amesema kuwa Jerop alikuwa anakwepa kuuliza maswali na wenzake na wakuu wake kazini kuhusu uwezo wake wa kukidhi kiwango fulani cha maisha.