Wafanyabiashara watatu mbaroni Iringa kwa utapeli

Jeshi la polisi mkoani Iringa linawashikilia wafanyabiashara watatu wa maduka yaliyopo mkabala na ofisi za mamlaka ya mapato TRA  ambayo yanajihusisha na vifaa vya maofisini kwa kushirikiana na baadhi ya maofisa wa TRA.

Kutoa leseni za udereva, kubadilisha kadi za umiliki wa vyombo vya moto bila kufuata utaratibu uliowekwa kisheria

Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Iringa ACP Allan Bukumbi amesema kuwakamatwa kwa watuhumiwa hao ni kutokana na kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema 

Amesema walipokea taarifa kuwa maeneo ya mtaa wa Mahiwa kata ya Gangilonga Manispaa ya Iringa kuna wafanyabiashara wa maduka yanajihusisha na vifaa vya maofisini wanashirikiana na watumishi  wawili wa TRA kutoa leseni na kuwapa wananchi bila kufuata utaratibu wa kisheria 

Aidha kamanda Bukumbi amesema Jeshi hilo linaendelea   kuwatafuta wenye leseni hizo za udereva na wamiliki wa namba za magari kwa kosa la kula njama na kujipatia leseni na namba  bila kufuata mfumo uliowekwa kwa mujibu wa sheria 

Watuhumiwa watafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika


Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii