Uturuki kuondoa mabaki ya majengo eneo la tetemeko

Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki imesema kuwa mataifa 95 yamejitolea kutoa msaada katika kazi ya kusafisha, kuondoa mabaki na kuvunja majengo yanayoonekana kuhatarisha usalama wa watu kurejesha eneo lililoathirika katika hali ya kawaida.

Taarifa hiyo imesema zaidi ya waokoaji 110,000 watakuwa tayari sambamba na upatikanaji wa vifaa muhimu kwa ajili ya kazi hiyo ikiwamo trekta na mashine za kuchimbia.

Hali ya baridi kali, ndiyo iliyoongeza ugumu wa utafutaji wa majeruhi na kufifisha matumaini ya kupatikana majeruhi zaidi pamoja kuwa timu ya wataalamu walisema, kuna uwezekano wa majeruhi kuhimili kwa muda wa wiki moja au zaidi.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii