Mamlaka za Usalama nchini Chad, zitaanza kuwasikiliza waasi 150 wanaotuhumiwa kusababisha kifo cha Rais Idriss Déby, katika Gereza la Kléssoum, lenye ulinzi mkali, ambao wanashtakiwa kwa ugaidi, kuandikisha watoto askari, utumwa, kudhoofisha usalama wa serikali, na mauaji ya rais.
Washukiwa hao ni kutoka chama cha Front for Concord and Change in Chad (FACT), lenye vuguvugu la waasi ambalo lilianzisha mashambulizi ya kuipindua serikali ya Chad kutoka kambi zake za nyuma nchini Libya mwaka 2021.