AJALI YA GARI YAUWA WATU WATANO PAPO HAPO MIKUMI

Watu 5 wamefariki dunia papo papo Mikumi Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro katika ajali iliyohusisha gari ndogo maarufu kama "IT"  iliyokuwa ikitokea  Bandarini Jijini Dar-es-salaam kuelekea  mpakani Tunduma  baada ya   kugongana  uso kwa uso na gari kubwa la mafuta  aina ya Benzi  iliyokuwa ikitokea Mkoani Iringa kuelekea Mkoani Morogoro.

Akithibitisha ajali hiyo, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Morogoro FORTUNATUS MUSILIMU amesema ajali hiyo iliyotokea majira ya  usiku wa kuamkia Jumatatu eneo la  IYOVI wilayani Kilosa  Mkoani Morogoro  katika barabara kuu ya  Morogoro-Iringa na kusema imesababishwa na  uzembe wa dereva wa wa gari ndogo ambaye inasemekana alikuwa akiendesha kwa kasi na gari likamshinda katika kona na kuvamia lori hilo.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii