Mtoto wa umri wa Miaka 6 ampiga risasi mwalimu wake

Mtoto mwenye umri wa miaka sita, anashikiliwa  na polisi baada ya kumpiga risasi mwalimu wake katika jimbo la Virginia nchini Marekani. 

Kwa mujibu wa ripoti ya maafisa wa polisi, mtoto huyo wa kiume alikamatwa baada ya kumpiga risasi mwalimu wake katika Shule ya Msingi ya Richneck mjini Newport News mnamo Ijumaa, Januari 6.

Mkuu wa Polisi wa eneo hilo Steve Drew alisema kuwa mwalimu huyo wa kike ambaye ana umri wa miaka 30, alipigwa risasi ndani ya darasa na kuongeza kuwa haikuwa tukio la bahati mbaya. 

Drew alisema kulikuwa na majibizano kati ya mwalimu na mwanafunzi hyo, ambaye alikuwa na bunduki, na kwamba risasi moja ilipigwa. 

Mwalimu huyo ambaye jina lake lilibanwa, alipata majeraha mabaya ambayo yanahatarisha maisha yake na alikimbizwa katika hospitali ya eneo hilo ambapo anafuatiliwa kwa karibu na madaktari. Bado haijulikani ni vipi mtoto huyo alipata bunduki hiyo. "Tutafanya uchunguzi, kuna maswali tutataka kuuliza na kujua. Nataka kujua hiyo bunduki ilitoka wapi, hali ilikuwaje,” Drew aliongeza.

Jambo la kushangaza ni kwamba shule hiyo ambayo ina wanafunzi wapatao 550 ilikuwa na vifaa vya kugundua chuma ikiwemo silaha na wanafunzi walikaguliwa bila mpangilio hivyo kila mtoto hakukaguliwa. Afisa anayesimamia Shule katika eneo hilo, Dkt. George Parker alisema Shule ya Msingi ya Richneck itafungwa Jumatatu, Januari 9. "Nimeshtuka, na nimevunjika moyo. Tunahitaji kuelimisha watoto wetu na tunahitaji kuwaweka salama.

Tunahitaji kuungwa mkono na jamii, kuendelea kuungwa mkono, ili kuhakikisha kuwa bunduki hazipatikani kwa vijana na ninasikika kama rekodi iliyovunjika leo, kwa sababu ninaendelea kusisitiza kwamba: tunahitaji kuzuia bunduki kutoka kwa mikono ya watu. vijana wetu,” alisema Parker katika kikao na wanahabari 

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii