Kamanda Jongo ameendelea kuwaomba wananchi kutoa taarifa pale wanapokuwa na mashaka na mtu kufanya vitendo vya kikatili ili kupunguza vitendo hivyo na kupata jamii iliyo salama.
"Ni kitendo Kibaya, kitendo cha kikatili sana na mbaya zaidi kilitokea kipindi cha siku 16 za kupinga ukatili, kwahiyo huo ni moja ya ukatili ambao unatokea, kwahiyo niisihi jamii pale wanapowaona mabinti na maisha ambayo hayampendezi Mungu na maisha ambayo hayapendezi jamii na maisha ambayo yapo kinyume na sheria na kanuni za nchi yetu ni vema kutoa taarifa," ameongeza Kamanda Jongo