Shirika la haki za binadamu la Human Rights Watch limesema leo kuwa
kundi la waasi wa M23 liliwatuhumu na kuwaua raia 29 pasina kuwapa fursa
ya kujitetea tangu katikati mwa Juni, katika maeneo yalioko chini ya
udhibiti wao. Shirika hilo limesema mashuhuda waliliambia kuwa Juni 21,
kufuatia mapigano karibu na kijiji cha Ruvumu, M23 iliwauwa raia
wasiopungua 17, wakiwemo watoto wawili, waliowatuhumu kwa kutoka taarifa
kwa jeshi la Congo kuhusu ngome na maficho ya waasi hao. Limesema
baadhi ya wahanga walipigwa risasi wakati wanajaribu kukimbia, huku
wengine wakipigwa risasi kwa karibu. Vifo vingine vilitokea katika
mashambulizi yaliofuatia kwenye kijiji sawa na katika vijiji vidogo vya
Ruseke na Kabindi, na hivyo kufikisha idadi ya vifo kuwa 29. Mwezi
uliyipita wapiganaji wa M23 waliuteka mji wa kimkakati wa Bunagana,
kwenye mpaka wa Congo na Uganda. Serikali ya Congo inashtumu Rwanda kwa
kuwaunga mkono waasiwa M23, madai ambayo serikali mjini Kigali
inayakanusha.
Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii