Jeshi la Polisi Mkoani Iringa
limefanikiwa kumkamata Mtuhumiwa na Mfanyabiashara Kaloli Mkusa mwenye
umri wa miaka 30 ambaye alihukumiwa kwenda Jela miaka 30 na fidia ya
shilingi million moja kwa kosa la kumbaka mama yake Mzazi katika kijiji
cha kisisina.
Mkusa ambaye alikuwa akifanya biashara Tunduma mkoani Songwe
alihukumiwa wiki moja iliyopita huku akiwa ametoweka kusikojulikana
kutokana yeye pamoja na baba yake mzazi Joseph Mkusa ambaye alimuwekea
Dhamana.