anajeshi wawili wanaodaiwa kuwa wa Rwanda waliokamatwa katika mpaka wa DRC na nchi hiyo wametambulishwa kwa wanahabari .
Koplo Élysée Nkundabangezi na Pte Ntwari Gad walikamatwa na wakazi wa Bwisha, kilomita 20 kutoka mpaka wa Rwanda alisema JeneralI Sylvain Ekenge, msemaji wa jeshi wa mkoa wa Kivu-Kaskazini.
Msemaji huyo wa jeshi aliongeza kuwa wanajeshi hao wawili wa Jeshi la Ulinzi la Rwanda (RDF) waliingia DRC, Jumatano iliyopita ili kushambulia kambi ya kijeshi ya Runangabo, kabla ya kukamatwa na watu.
Taarifa iliyotolewa na Jeshi la ulinzi la Rwanda (RDF) hapo jana iliomba kuachiliwa kwa wanajeshi hao waliotekwa nyara wakiwa kwenye doria na Vikosi vya Wanajeshi wa DRC na FDLR [kundi la waasi lenye asili ya Rwanda], baada ya uvamizi katika ardhi ya Rwanda Mei 23, 2022.
Hivi majuzi serikali ya Congo iliishutumu Rwanda kwa kusaidia kundi la wanamgambo wa M23, tuhuma ambazo Rwanda inakanusha, lakini badala yake, kama ilivyokaririwa katika barua hiyo, inaishutumu DRC kwa kushirikiana na FDLR, ambayo inatuhumiwa kufanya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 nchini Rwanda.
Mapigano mapya yalizuka kati ya FARDC na M23[Kundi linaloongozwa na Watutsi wa Kongo] yameleta biashara ya shutuma za mashambulizi kati ya Rwanda na DRC, huku nchi zote mbili zikilaumiana kuunga mkono makundi yao yenye silaha yaliyoasi.
Karibu watu 37,000 wamekimbia makazi yao kutokana na mapigano ya hivi karibuni, kulingana na Baraza la Wakimbizi la Norway.