Mwizi Avamia Kambi ya Kijeshi Kiambu na Kuiba Bunduki Wanajeshi Wakioga.

Polisi mjini Thika katika kaunti ya Kiambu wameanzisha msako wa kumsaka mwanamume asiyejulikana ambaye alivamia kambi ya Thika Barracks na kuiba bunduki.
Kisa hicho kilitokea Jumatatu, Aprili 25, katika kambi ya Twelve Engineer Battalion Thika Barracks mnamo Jumatatu, Aprili 25 mwendo wa saa kumi na mbili jioni.
Kulingana na taarifa ya polisi, mwanamume huyo aliingia kwenye eneo la kusubiri, kuvunja dirisha na kuiba bunduki aina ya AK 47 iliyokuwa na risasi 30.
Kisa hicho kiliripotiwa na maafisa wawili, John Kibaki na Alvin Nyasio, waliokuwa wanahudumu katika kambi hiyo.
Wawili hao waliambia wachunguzi kwamba kisa hicho kilitokea walipokuwa wameenda kuoga mita kadhaa, na kuacha kituo bila ulinzi.
"Ofisa huyo alikuwa akifanya kazi na watu wengine wanne kwenye kituo hicho na wakati wa tukio hilo, hakuna aliyekuwa kazini walikuwa wamekwenda wote kuoga kwenye jengo lililo umbali wa mita 400 kutoka kituo hicho," ilisoma ripoti ya polisi kwa sehemu.
Bunduki hiyo ilikuwa imepewa afisa Kenneth Mbae.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii