Twitter Yawatimua Kazi Mameneja Wawili Kupisha Utawala wa Elon Musk

TWITTER imewatimua kazi Mameneja wawili wa ngazi ya juu na kusitisha ajira ikiwa ni mpango wake wa mabadiliko chini ya utawala mpya wa bilionea namba moja duniani Elon Musk.

Mtandao huo wa kijamii umethibitisha kuondoka kwa Meneja Mkuu Kayvon Beykpour na Mkuu wa bidhaa na kodi Bruce Falck na kusisitiza kuwa ajira itauwa ni kwenye maeneo muhimu tu huku ikisubiri kipindi cha mabadiliko chini ya utawala wa Elon Musk.

Wote wawili walithibitisha kuwa wameondolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Twitter Parag Agrawal.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii