Kumekuwa na hisia kali baada ya taarifa za kifo cha mwimbaji wa nyimbo za Injili kutoka Nigeria Osinachi Nwachukwu.
Ripoti za awali zilisema kuwa mwanadada huyo mwenye umri wa miaka 42 alikuwa anaugua saratani ya koo, lakini familia yake inakanusha hilo, kwa madai kuwa alikuwa mwathirika wa unyanyasaji wa nyumbani.
Mumewe Peter Nwachukwu amekamatwa na polisi, na bado hajazungumza lolote.
“Pumzika kwa amani mwana wa Mungu, nilipenda jinsi alivyomwabudu Mungu,” alisema shabiki wa Afrika Kusini, Hilda Motswatswa.
Abel Phanuel akiwa Lagos aliandika: "Moyo wangu uko pamoja na familia yake katika nyakati hizi za majaribu. #SemaNoToDomesticViolence."
"Kwa kweli alitoa moyo wake katika wimbo wa Ekuweme," alisema Caren Akoth, "labda ilikuwa njia yake ya kuelezea huzuni zake".
Na huko Liberia, David Jacque Tarpeh aliandika: "Huu ni wakati wa wanawake wote wa Nigeria kukusanyika pamoja na kudai haki kwa kufanya maandamano ya amani".