Mamilioni ya waumini wa dini ya Kikristo duniani leo wanasherehekea sikukuu ya Pasaka kukumbuka kufufuka kwa Yesu Kristo baada ya kusulubiwa msalabani zaidi ya miaka 2000 iliyopita. Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, ameutumia ujumbe wake wakati wa misa ya mkesha wa Pasaka kulaani kile amekitaja ukatili wa vita unaoshuhudiwa nchini Ukraine. Bila kuitaja moja kwa moja Urusi, Baba Mtakatifu ametoa wito wa kuwepo usitishaji mapigano katika siku ya leo ya Pasaka kwa malengo ya kufikia makubaliano ya amani kwa njia ya mazungumzo. Sikukuu ya Pasaka, ambayo ni miongoni sherehe muhimu katika kalenda ya dini ya Kikristo, husherehekewa kila mwaka kwa waumini kuhudhuria misa, kuandaa karamu na wengine kutembeleana.